Kutafuta mapinduzi Senegal

Maisha ya mwanaharakati na msanii wa Senegal Omar Blondin Diop yatasaidia kutoa mtazamo wa jinsi siasa za kiukombozi zilivyo katika ukoloni mamboleo.

Omar Blondin Diop reading the Internationale situationniste. Image credit Vincent Meessen via Bouba Diallo.

Mwaka 2013, familia ya Omar Blondin Diop ilifanya utaratibu wa sherehe ya kumbukizi yake, ya miaka arobaini baada ya kifo chake kilichotokea eneo la Gorée. Kwa karne nzima, kisiwa hiki kilikuwa kama kitovu kwa njia ya meli za watumwa waliokamatwa sehemu mbalimbali Afrika kupelekwa Marekani. Kama sehemu ya maadhimisho ndugu zake waliweka picha wake kwenye kizimba alichokuwa amefungwa ndani ambapo sasa ni sehemu muhimu ya maonyesho katika Jumba la Makumbusho la Senegal. Picha hiyo ilimwonyesha katika mwaka wa 1970, mara tu alipofukuzwa kutoka Ufaransa ambapo alikuwa akiishi kwa mwongo mzima. Picha hii ilipochukuliwa, alikuwa mwanafunzi wa Shahada ya udhamifu, akiwa na umri wa miaka 23; katika filosofia. Kama walivyokuwa wanafunzi wengi katika mwaka ule, alikumbana na kadhia ya uasi ya mwaka 1968. Lakini miaka mitano baadaye akiwa mpinzani mashuhuri ; Omar Blondin Diop alibaki kuwa hadithi tu. Alipokufa gerezani, miezi kumi na minne baada ya kuhukumiwa kwenda gerezani kama mfungwa kwa miaka mitatu kama mtu hatari sana kwa usalama wa taifa, Mamlaka za Senegal zilidai kwamba alijiua. Lakini wengi walikuwa na sababu nzuri za kuamini kwamba aliuwawa. Na tokea wakati huo, familia yake, bila kuchoka ilitaka haki itendeke, na wasanii pamoja na wanaharakati wengi wamekuwa mstari wa mbele kushikilia kumbukumbu yake.

Kuuawa kwa Omar Blondin Diop, hakuwezi kueleweka kama tukio tu la pekee, lakini kama vipindi vingi vya huzuni katika mfululizo wa ukandamizaji, na uzuiaji wa demokrasia nchini Senegal. Upinduzi kutoka wakoloni umekuwa ni hadithi ya kawaida kwa kuzaliwa kwa mataifa huru bara la Afrika haswa kuanzia mwongo wa 1960. Hata hivyo kushikiliwa kwa maslahi ya Serikal za kimataifa bado ni sura halisi ya mataifa yote yaliyokuwa chini ya Ukoloni wa Kifaransa. Hata hivyo katika uhuru uliotajwa tu kisiasa, kuchipuka kwa utawala wa kidikteta (utawala wa mtu mmoja) kwa sehemu kubwa kumedumaza dhana ya mapinduzi ya ukombozi kutoka kwenye ubeberu na ubepari. Hatusikii sana vikundi vya upinzani Senegali wakati wa Leopald Sedar Senghor aliyetawala kati ya 1960-1980 kwa sababu mfumo wa utawala wake ulifanikiwa kuichora nchi hiyo kama nchi yenye demokrasia iliyofanilikiwa Afrika. Lakini katika mfumo wa chama kimoja cha Progressive Senegalese Union, mamlaka zilipanga njia ovu za ukatili ; kama vile kuwakamata watu, kuwafunga, kuwatisha, kuwatesa na hata kuwaua. Omar Blondin Diop alikuwa miongoni mwao waliotekwa.

Omar Blondin Diop alizaliwa koloni la Ufaransa la Niger mnamo mwaka 1946. Baba yake alikuwa ni muuguzi na alihamishwa kutoka Dakar, mji wa kiutawala wa Ufaransa kwa Afrika ya Magharibi, na kupelekwa kwenye mji mdogo wa Niamey. Ingawa hakuwa na nafasi yoyote katika miungano ya mapinduzi, mamlaka za kikoloni zilimshuku kuwa ni mpinzani wa maono au mawazo ya Wafaransa kwa sababu ya kujihusisha kwake na chama cha wafanyabiashara na kusaidia katika kitengo cha kijamii katika chama cha kimataifa cha wafanyakazi. Ofisi za wakoloni katika mji mkuu Ufaransa zilifuatilia chochote kilichosemekana kupingana na Ufaransa kwa sababu ya hofu kwamba vikundi vinavyopinga ukoloni vingeeneza taabu. Wakati ambapo familia ya Blondin Diop waliruhusiwa kurudi Senegali, aliishi miaka mingi ya utoto wake katika jiji la Dakar. Alipokuwa na umri wa miaka 14 alihamia Ufaransa, ambapo baba yake alijihusisha kwenye Shule ya udaktari.

Katika mwongo huo wa 1960, Blondin Diop aliishi Ufaransa. Maisha yake wakati wa elimu ya Sekondari yalikuwa Ufaransa, ambapo alihudhuria Chuo cha hadhi cha Ualimu, na kuhitimu katika elimu ya tamaduni za Ulaya na matabaka. Alipokuwa chuoni, Blondin Diop alianza kama mwanasiasa mwenye mlengo wa kushoto. Huu ulikuwa wakati ambapo vikundi vya kupinga ubepari vilianza kuwa hai kuanzia kwenye tamaduni za kimapinduzi za China, na kupinga kwa nguvu zote uvamizi wa Amerika nchini Vietnam. Kwa kawaida Waafrika ambao walijiingiza kwenye harakati huko Ufaransa, walikuwa na mitazamo ya kisiasa kutoka kwenye nchi zao wenyewe. Blondin Diop, kwa nafasi yake alikuwa na sehemu pande zote mbili. Muda mfupi baada ya kusikia kuhusu mwanaharakati huyu aliyetoka Senegali, mtengeza filamu mashuhuri Jean-Luc Godard alimchagua Blondin Diop kushiriki kwenye filamu yake iliyoitwa La Chinoise (1967). Mnamo 1968, akiwa mwanafunzi-mwalimu wa miaka ishirini na moja, alishiriki kikamilifu kwenye mdahalo ulio tayarishwa na makundi mengine ya mlengo wa kushoto. Akihuishwa na maandiko ya Spinoza, Marx, na Fanon, akajikita katika kutafuta msimamo wowote ndani na nje ya uhalisia, utawala huria, nadharia ya siasa na matendo ya Mao Tse-Tung. Hakujiweka kando na itikadi moja fulani.

Kwa sababu ya harakati zake katika siasa, Blondin Diop alifukuzwa Ufaransa na kurudishwa Senegali mwishoni mwa mwaka 1969. Pamoja na marafiki zake wengine waliosoma naye Ulaya, alishiriki katika harakati za Vijana wa Marxist-Leninist. Kundi hilo baadaye likazaa kundi lingine lililoshawishi sana umoja dhidi ya ubeberu And Jëf (Kufanya Kazi Pamoja), ambalo lililazimishwa kujificha mpaka mwanzoni mwa mwongo wa 1981. Waliporudisha mfumo wa awali, Blondin Diop alikuza maonesho ya sanaa. Alianzisha mradi wa “Tamthilia mitaani ambayo ingeshughulikia maswala na maslahi ya wananchi” kufanana na tamthilia ya Augusto Boal “Tamthilia ya Wananchi Waliokandamizwa.” Alipotanuka katika sanaa muhimu ya kimapinduzi, Blondin Diop aliandika:

Tamthilia yetu itakuwa ya ubunifu wenye hamasa mchanganyiko. Kabla ya kuchezwa kwa majirani zetu, tutajua washiriki wake, tutatumia muda mwingi pamoja nao, haswa vijana […]. Tamthilia yetu itapelekwa sehemu ambazo zitakuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu (masokoni, majumba ya sinema, viwanja vikubwa) […]. Ni muhimu tufanye kila liwezekanalo wenyewe […]. Hitimisho la haki; Ni bora kifo kuliko utumwa.

Senegali huru bado ilikuwa ni eneo la Ukoloni mamboleo. Senghor awali alikuwa amepinga uhuru wa mapema, akijitetea badala yake kuwa na uwezo wa kujitawala kwa zaidi ya miaka ishirini. Hivyo alipokuwa Rais, mara kwa mara alikuwa akiomba misaada kwa Ufaransa. Mwaka 1962 Senghor aliropoka kumlaumu mshirika mwenzake wa muda mrefu Mamadou Dia, Rais wa baraza la mawaziri la Senegali kwa jaribio la kutaka kumpindua. Baadaye Dia alikamatwa na kuwekwa kifungoni kwa zaidi ya miaka kumi. Mwaka 1968 wakati mgogoro mkubwa wa Uma ulipolipuka katika jiji la Dakar, polisi waliwakandamiza waandamanaji kwa msaada wa vikosi vya Ufaransa. Mwaka 1971 kujishikamanisha kwa Senghor na Ufaransa, kulionekana kufikia kileleni kwa ujio wa Rais wa Ufaransa Georges Pompidou, rafiki wa karibu na rafiki waliosoma naye darasa moja. Kwa zaidi ya mwaka mmoja jiji la Dakar lilikuwa likiandaliwa kwa mapokezi na ujio wa Pompidou wa saa 24 tu. Katika njia yote ya msafara, mamlaka zilifanya matengenezo ya barabara na majengo, zikijaribu kuficha umasikini wa jiji.

This map retraces Omar Blondin Diop’s main travels (1946-1973). Image credit Florian Bobin and Tristan Bobin (click for larger view).

Kwa wanaharakati vijana wabobezi, mapokezi ya Rais wa Ufaransa Senegali yalikuwa uchokozi wa wazi. Wiki chache kabla ya ujio huo kundi lililohamasishwa na makundi mawili ya American Black Panther na Uruguayan Tupamaros walichoma moto kituo cha utamaduni cha Ufaransa kilichopo jijini Dakar. Walipojaribu kuingilia msafara wa Rais, walikamatwa. Miongoni mwao walioonekana na hatia, wawili walikuwa ndugu zake Blondin Diop. Ingawa aliegemeza matukio haya ya uoinduzi, hakuhusika kwenye mipango. Alikuwa amerejea Paris miezi michache kabla, baada ya kibali chake cha kuingia kupigwa marufuku. Akiwa na huzuni, Blondin Diop aliamua akiwa na marafiki zake wa karibu, kuondoka Ufaransa kwenda kujifunza mapambano ya silaha. Wakapanda chombo kuelekea mashariki, wakapita Ulaya yote kwa gari moshi kabla ya kufika kwenye kambi za Syria walipoungana na wapiganaji wa Kipalestina, na askari wa msituni wa Eritrea. Mpango wao ukiwa ni kumteka nyara balozi wa Ufaransa nchini Senegali, ili wabadilishane na rafiki zao waliokuwa wamefungwa gerezani.

Miezi miwili katika mafunzo ya kijeshi, Blondin Diop na washiriki wake wakatoka jangwani kwenda jijini. Walitumaini kupata msaada wa silaha kutoka kwenye kundi la Black Panther Party, ambao walikuwa wamefungua ofisi ya kimataifa katika jiji la Algiers. Hata hivyo, mgawanyiko kwenye kundi lao, uliwalazimisha kuwaza upya. Baada ya kuyumbishwa Conakry walienda kupiga kambi Bamako ambapo sehemu ya familia ya Blondin Diop iliishi. Na kutokea hapo wakajipanga upya.

Mwezi wa kumi na moja mwaka 1971, Polisi walilikamata kundi hilo siku chache kabla ya ziara ya kwanza ya kitaifa ya Rais Senghor nchini Mali. Watu wa intellejensia wa usalama, walikuwa wakiwafuatilia kwa miezi kadhaa. Mfukoni mwa Blondin Diop, walikuta barua iliyoeleza mpango wa kundi hilo, kuwatoa rafiki zao wengine waliokuwa wamefungwa. Aliporejeshwa Senegali alihukumiwa miaka mitatu jela. Kwa umaalumu katika siku zao walipokuwa kwenye vizimba vyao, hawakuruhusiwa kutoka humo. Kupunguza mwingiliano, mwonjo wa mchana ulipunguzwa – wafungwa waliruhusiwa nuru nusu saa tu asubuhi, na nusu saa mchana. Siku zote zilikuwa usiku tu; na usiku ulikuwa hauishi, na mateso yalikuwa ni kawaida.

Omar Blondin Diop aliripotiwa kufariki tarehe 11 mwezi wa tano 1973, akiwa na miaka 26. Taarifa zilitoka kama mlipuko wa bomu. Mamia ya vijana wakafurika mitaani, wakaandika kwenye kuta za jiji “Senghor, katili; wanauwa watoto wenu, amka; Makatili, Blondin ataishi.”

Tangia awali kabisa, Serikali ya Senegali ilificha uhalifu. Kwenda kinyume na maagizo rasmi, majaji waliokuwa wanachunguza wakawashtaki washukiwa wawili. Katika kitabu cha gereza ilionyesha kwamba Blondin Diop alikuwa amezimia tangu siku moja kabla ya kutangazwa kwake kuwa ameaga dunia. Hata hivyo, utawala wa gereza ulikuwa haujafanya lolote. Kabla jaji kupata muda na nafasi ya kumkamata mshukiwa wa tatu, mamlaka zilimbadilisha jaji na kufunga jalada hilo. Kila mwezi wa tano tarehe 11 hadi miaka ya tisini, vikosi vya askari vyenye silaha vilizunguka kaburi lake kuzuia aina yoyote ya kumbukizi yake.

Kwa miongo kadhaa, Omar Blondin Diop amekuwa chanzo cha chachu kwa wanaharakati wengi na wasanii huko Senegali, na kwingine duniani. Katika miaka ya karibuni, maonyesho, michoro, na maigizo yamehusisha simulizi yake ambayo kwa huzuni nyingi inatetema sambamba na siasa. Njia za kimamlaka zinazotumika na uongozi wa sasa wa Senegali zinaonyesha kuepuka adhabu ya zamani. Mfumo wa utawala wa Raisi Macky Sall, mara kwa mara umetafuta kukandamiza uhuru wa maandamano, ubadhilifu wa fedha za Umma, na kutumia vibaya mamlaka yake. Na kwa kuwa uwajibikaji wa Serikali hauna kusudi lingine lolote isipokuwa kuvutia misaada ya kimataifa, tabia zilezile za kitambo zinadumu kuishi na kuendelea hata sasa. Hata leo Senegali watu wanafungwa jela wakijaribu kuandamana. Wanaharakati kama Guy Marius Sagna bado wana teswa, wanakamatwa na kinyume cha sheria wanafungwa. Katika mazingira hayo, na kwa mshangao, bado Serikali imegoma kufungua kwa upya kesi ya Omar Blondin Diop. Hata hivyo, familia yake inashikilia kuwa “haijalishi muda mrefu wa usiku, jua ni lazima litachomoza tu.”

Further Reading

The Senghor myth

Once you’ve exhausted all the Negritude quotes, you have to confront the fact that Leopold Sedar Senghor ran Senegal as a repressive, one-party state.